Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 7:7-15 Biblia Habari Njema (BHN)

7. “Lakini mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Jambo hilo halitafaulu kamwe.

10. Tena Mwenyezi-Mungu akamwambia Ahazi,

11. “Mwombe Mwenyezi-Mungu, Mungu wako, akupe ishara; iwe ni kutoka chini kuzimu au juu mbinguni.”

12. Ahazi akajibu, “Sitaomba ishara! Sitaki kumjaribu Mwenyezi-Mungu.”

13. Basi, Isaya akamjibu, “Sikiliza basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Je, haitoshi kuwachosha watu hata sasa mnataka kumchosha Mungu wangu pia?

14. Haya basi, Bwana mwenyewe atawapa ishara: Msichana atachukua mimba, atajifungua mtoto wa kiume na kumwita jina lake Emanueli.

15. Atakula siagi na asali mpaka atakapojua kukataa mabaya na kuchagua mema.

Kusoma sura kamili Isaya 7