4. Tangu kale hakuna aliyepata kuonawala kusikia kwa masikio yake;hakuna aliyepata kumwona Mungu aliye kama weweatendaye mambo kwa ajili ya wale wanaomtegemea!
5. Wewe waja kuwasaidia watendao haki kwa furaha,wanaokukumbuka na kuzingatia njia zako.Ulitukasirikia tulipokuwa wenye dhambi;sisi tumeasi kwa muda mrefu.
6. Sote tumekuwa kama watu walio najisi;matendo yetu yote mema ni kama nguo chafu.Sote tunanyauka kama majani,uovu wetu watupeperusha kama upepo.
7. Hakuna hata mmoja anayekuja kukuomba;hakuna anayejishughulisha kukutafuta.Wewe unauficha uso wako mbali nasi,umetuacha tukumbwe na maovu yetu.
8. Hata hivyo, ee Mwenyezi-Mungu, wewe ni Baba yetu.Sisi ni kama udongo, wewe ni mfinyanzi.Sisi sote ni kazi ya mikono yako.
9. Usitukasirikie mno, ee Mwenyezi-Mungu,usiukumbuke uovu wetu daima!Ukumbuke kwamba sisi sote ni watu wako!
10. Miji yako mitakatifu imekuwa nyika;Siyoni umekuwa mahame,Yerusalemu umekuwa uharibifu.
11. Nyumba yetu takatifu na nzuri,ambamo wazee wetu walikusifu,imeteketezwa kwa moto.Mahali petu pote pazuri pamekuwa magofu.