Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 63:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu,anayefika kutoka Bosra na mavazi ya madoa mekundu?Ni nani huyo aliyevaa mavazi ya fahari,anatembea kwa nguvu zake kubwa?Ni mimi Mwenyezi-Munguninayetangaza ushindi wangu;nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.

2. Lakini mbona nguo yako ni nyekundu,nyekundu kama ya mtu anayekamua zabibu?

3. “Naam, nimekamua zabibu peke yangu,wala hakuna mtu aliyekuja kunisaidia.Nimeyakanyaga mataifa kwa hasira yangu,niliyapondaponda kwa ghadhabu yangu.Nguo zangu zimejaa madoa ya damu yao,imeyachafua kabisa mavazi yangu.

4. Niliamua kuwa siku ya kulipiza kisasi imefika;wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.

5. Nilitazama na hapakuwa na wa kunisaidia;nilishangaa hapakuwa na wa kuniunga mkono.Lakini nilijipatia ushindi kwa mkono wangu,ghadhabu yangu ilinihimiza.

6. Kwa hasira yangu niliwaponda watu,niliwalewesha kwa ghadhabu yangu;damu yao niliimwaga chini ardhini.”

7. Nitasimulia fadhili za Mwenyezi-Mungu;nitataja matendo yake yote yastahiliyo sifa,kwa sababu ya yote aliyotutendea,wema wake mkuu aliowapa Waisraeli kwa huruma yake,kadiri ya wingi wa fadhili zake.

Kusoma sura kamili Isaya 63