Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 62:9-12 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Bali nyinyi mliyoivuna nafaka hiyo,mtaila na kunitukuza mimi Mwenyezi-Mungu.Nyinyi mliochuma zabibu hizo,mtakunywa divai yake katika nyua zangu takatifu.”

10. Wakazi wa Yerusalemu, tokeni, tokeni nje ya mji,watayarishieni njia watu wenu wanaorejea!Jengeni! Jengeni barabara na kuondoa mawe yote!Wekeni alama kwa ajili ya watu.

11. Mwenyezi-Mungu ametangaza duniani kote,waambie watu wa Siyoni:“Mkombozi wenu anakuja,zawadi yake iko pamoja nayena tuzo lake liko mbele yake.”

12. Nyinyi mtaitwa: “Watu Watakatifu”,“Watu waliokombolewa na Mwenyezi-Mungu.”Na Yerusalemu utaitwa: “Mji aupendao Mungu”,“Mji ambao Mungu hakuuacha.”

Kusoma sura kamili Isaya 62