Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 60:11-15 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Malango yako yatakuwa wazi daima;usiku na mchana hayatafungwa,ili watu wakuletee utajiri wa mataifa,pamoja na wafalme wao katika maandamano.

12. Kila ufalme au taifa lisilokutumikia litaangamia;mataifa hayo yatatokomezwa kabisa.

13. “Utaletewa fahari ya msitu wa Lebanoni:Mbao za miberoshi, mivinje na misonobari,zitumike kupamba mahali pa maskani yangu;nami nitaparembesha hapo ninapokaa.

14. Wazawa wa wale waliokudhulumu,watakuja na kukuinamia kwa heshima.Wote wale waliokudharau,watasujudu mbele ya miguu yako.Watakuita: ‘Mji wa Mwenyezi-Mungu’,‘Siyoni, Mji wa Mtakatifu wa Israeli’.

15. “Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa,hakuna aliyependa hata kupitia kwako.Lakini sasa nitakufanya uwe na fahari milele,utakuwa mji wa furaha kizazi hata kizazi.

Kusoma sura kamili Isaya 60