3. Maana mikono yenu imetiwa najisi kwa mauaji,na vidole vyenu kwa matendo maovu.Midomo yenu imesema uongo,na ndimi zenu husema uovu.
4. Hakuna atoaye madai yake kwa haki,wala anayeshtaki kwa uaminifu.Mnategemea hoja batili;mnasema uongo.Mnatunga hila na kuzaa uovu.
5. Mnaangua mayai ya joka lenye sumu,mnafuma utando wa buibui.Anayekula mayai yenu hufa,na yakipasuliwa nyoka hutokea.
6. Utando wenu haufai kwa mavazi,watu hawawezi kujifunikia mnachofuma.Kazi zenu ni kazi za uovu,matendo yenu yote ni ukatili mtupu.