Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 59:12-21 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Makosa yetu mbele yako ni mengi mno,dhambi zetu zashuhudia dhidi yetu.Naam, makosa yetu tunaandamana nayo,tunayajua maovu yetu.

13. Tumekuasi na kukukana ee Mwenyezi-Mungu,tumekataa kukufuata ewe Mungu wetu.Udhalimu na uasi ndivyo tunavyopania,mioyoni mwetu twatunga na kutoa maneno ya uongo.

14. Haki imewekwa kando,uadilifu uko mbali;ukweli unakanyagwa mahakamani,uaminifu haudiriki kuingia humo.

15. Ukweli umekosekana,naye anayeacha uovu hunyanyaswa.Mungu aliona mambo hayo, akachukizwa,alichukizwa kwamba hakuna haki.

16. Aliona kwamba hakuna mtu aliyejali,akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati.Basi akaamua kunyosha mkono wake mwenyewe,uadilifu wake ukamhimiza.

17. Alivaa uadilifu kama vazi la kujikinga kifuani,na wokovu kama kofia ya chuma kichwani.Atajivika kisasi kama vazi,na kujifunika wivu kama joho.

18. Atawaadhibu maadui kadiri ya matendo yao,naam, ghadhabu yake na kisasi vitawapata maadui zake;atawaadhibu hata wakazi wa nchi za mbali.

19. Toka magharibi hadi mashariki,kila mtu atamcha Mwenyezi-Munguna kutambua utukufu wake.Maana atakuja kama mto uendao kasi,mto unaosukumwa kwa upepo wa Mwenyezi-Mungu.

20. Naye atakuja Siyoni kama Mkombozi,Mkombozi wa wazawa wa Yakoboambao wataachana na makosa yao.Asema Mwenyezi-Mungu.

21. Mwenyezi-Mungu asema:“Mimi nafanya nanyi agano hili:Roho yangu niliyowajazeni,maneno niliyoyaweka mdomoni mwenu,hayataondoka kwenu kamwe,wala kwa watoto na wajukuu zenu,tangu sasa na hata milele.”

Kusoma sura kamili Isaya 59