Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 59:10-16 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Kama vipofu twapapasapapasa ukuta;tunasitasita kama watu wasio na macho.Tunajikwaa mchana kana kwamba ni usiku,miongoni mwa wenye nguvu sisi ni kama wafu.

11. Twanguruma kama dubu,twaomboleza tena na tena kama hua.Twatazamia hukumu ya haki, lakini haipo,twatazamia wokovu, lakini uko mbali nasi.

12. Makosa yetu mbele yako ni mengi mno,dhambi zetu zashuhudia dhidi yetu.Naam, makosa yetu tunaandamana nayo,tunayajua maovu yetu.

13. Tumekuasi na kukukana ee Mwenyezi-Mungu,tumekataa kukufuata ewe Mungu wetu.Udhalimu na uasi ndivyo tunavyopania,mioyoni mwetu twatunga na kutoa maneno ya uongo.

14. Haki imewekwa kando,uadilifu uko mbali;ukweli unakanyagwa mahakamani,uaminifu haudiriki kuingia humo.

15. Ukweli umekosekana,naye anayeacha uovu hunyanyaswa.Mungu aliona mambo hayo, akachukizwa,alichukizwa kwamba hakuna haki.

16. Aliona kwamba hakuna mtu aliyejali,akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati.Basi akaamua kunyosha mkono wake mwenyewe,uadilifu wake ukamhimiza.

Kusoma sura kamili Isaya 59