Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 59:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Msifikiri mkono wa Mungu ni mfupi,hata asiweze kuwaokoeni;au masikio yake yamezibika,hata asiweze kuwasikieni.

2. Dhambi zenu ndizo zinazowatenga na Mungu wenu,dhambi zenu zimemfanya ajifiche mbali nanyihata asiweze kuwasikieni.

3. Maana mikono yenu imetiwa najisi kwa mauaji,na vidole vyenu kwa matendo maovu.Midomo yenu imesema uongo,na ndimi zenu husema uovu.

4. Hakuna atoaye madai yake kwa haki,wala anayeshtaki kwa uaminifu.Mnategemea hoja batili;mnasema uongo.Mnatunga hila na kuzaa uovu.

5. Mnaangua mayai ya joka lenye sumu,mnafuma utando wa buibui.Anayekula mayai yenu hufa,na yakipasuliwa nyoka hutokea.

6. Utando wenu haufai kwa mavazi,watu hawawezi kujifunikia mnachofuma.Kazi zenu ni kazi za uovu,matendo yenu yote ni ukatili mtupu.

7. Mko mbioni kutenda maovu,mnaharakisha kumwaga damu isiyo na hatia.Mawazo yenu ni mawazo ya uovu,popote mwendapo mnaacha ukiwa na uharibifu.

8. Njia ya amani hamwijui kamwe;njia zenu zote ni za dhuluma.Mmejifanyia njia potovu,yeyote anayepitia humo hapati amani.

9. Ndio maana haki iko mbali nasi,maongozi ya uadilifu hayapo kwetu.Tunatazamia kupata mwanga kumbe ni giza tupu,twatazamia mwangaza, lakini twatembea gizani.

10. Kama vipofu twapapasapapasa ukuta;tunasitasita kama watu wasio na macho.Tunajikwaa mchana kana kwamba ni usiku,miongoni mwa wenye nguvu sisi ni kama wafu.

Kusoma sura kamili Isaya 59