Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 56:7-11 Biblia Habari Njema (BHN)

7. hao nitawaleta katika mlima wangu mtakatifu,na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala;tambiko na sadaka zao zitakubaliwa madhabahuni pangu.Maana nyumba yangu itaitwa:‘Nyumba ya sala kwa ajili ya watu wote’.

8. “Hii ni kauli yangu mimi Bwana Mwenyezi-Munguninayewakusanya Waisraeli waliotawanyika.Licha ya hao niliokwisha kukusanya,nitawakusanya watu wengine wajumuike nao.”

9. Enyi wanyama wote wakali,nanyi wanyama wote wa mwituni,njoni muwatafune watu wangu.

10. Maana viongozi wao wote ni vipofu;wote hawana akili yoyote.Wote ni kama mbwa bubu wasiobweka,hulala tu na kuota ndoto,hupenda sana kusinzia!

11. Hao ni kama mbwa wenye uchu sana,wala hawawezi kamwe kutoshelezwa.Wachungaji hao hawana akili yoyote;kila mmoja hutafuta faida yake mwenyewe.

Kusoma sura kamili Isaya 56