Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 52:7-14 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Tazama inavyopendezakumwona mjumbe akitokea mlimani,ambaye anatangaza amani,ambaye analeta habari njema,na kutangaza ukombozi!Anauambia mji wa Siyoni:“Mungu wako anatawala!”

8. Sikiliza sauti ya walinzi wako;wanaimba pamoja kwa furaha,maana wanaona kwa macho yao wenyewe,kurudi kwa Mwenyezi-Mungu mjini Siyoni.

9. Pazeni sauti za shangwe, enyi magofu ya Yerusalemu!Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,ameukomboa mji wa Yerusalemu.

10. Mwenyezi-Mungu ameonesha nguvu yake tukufu,mbele ya mataifa yote.Atawaokoa watu wake,na ulimwengu wote utashuhudia.

11. Ondokeni! Ondokeni! Tokeni hapa;msiguse kitu chochote najisi!Ondokeni huku Babuloni!Jitakaseni enyi mbebao vyombo vya Mwenyezi-Mungu.

12. Safari hii hamtatoka kwa haraka,wala hamtaondoka mbiombio!Maana Mwenyezi-Mungu atawatangulieni,Mungu wa Israeli atawalinda kutoka nyuma.

13. Mungu asema hivi:“Mtumishi wangu atafanikiwa;atatukuzwa na kupewa cheo,atapata heshima kuu.

14. Wengi waliomwona walishtuka,kwa vile sura yake ilikuwa imeharibiwa;hakuwa tena na umbo la kibinadamu!

Kusoma sura kamili Isaya 52