Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 52:11-15 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Ondokeni! Ondokeni! Tokeni hapa;msiguse kitu chochote najisi!Ondokeni huku Babuloni!Jitakaseni enyi mbebao vyombo vya Mwenyezi-Mungu.

12. Safari hii hamtatoka kwa haraka,wala hamtaondoka mbiombio!Maana Mwenyezi-Mungu atawatangulieni,Mungu wa Israeli atawalinda kutoka nyuma.

13. Mungu asema hivi:“Mtumishi wangu atafanikiwa;atatukuzwa na kupewa cheo,atapata heshima kuu.

14. Wengi waliomwona walishtuka,kwa vile sura yake ilikuwa imeharibiwa;hakuwa tena na umbo la kibinadamu!

15. Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi.Wafalme wanaduwaa kwa sababu yake,maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa,na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.”

Kusoma sura kamili Isaya 52