11. Ondokeni! Ondokeni! Tokeni hapa;msiguse kitu chochote najisi!Ondokeni huku Babuloni!Jitakaseni enyi mbebao vyombo vya Mwenyezi-Mungu.
12. Safari hii hamtatoka kwa haraka,wala hamtaondoka mbiombio!Maana Mwenyezi-Mungu atawatangulieni,Mungu wa Israeli atawalinda kutoka nyuma.
13. Mungu asema hivi:“Mtumishi wangu atafanikiwa;atatukuzwa na kupewa cheo,atapata heshima kuu.