19. Majanga haya mawili yamekupata:Uharibifu na maangamizi; njaa na mauaji.Nani atakayekuonea huruma?Nani atakayekufariji?
20. Watoto wako wamezirai,wamelala pembeni mwa kila barabara,wako kama paa aliyenaswa wavuni.Wamepatwa na ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu,wamepatwa na adhabu ya Mungu wako.
21. Basi, sikiliza ewe Yerusalemu unayeteseka;sikiliza wewe uliyelewa, lakini sio kwa divai.
22. Bwana, Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,awateteaye watu wake, asema hivi:“Nimekuondolea kikombe cha kuyumbisha,hutakunywa tena kikombe cha ghadhabu yangu.
23. Nitawanywesha watesi wako kikombe hichowaliokuambia ulale chini wapite juu yako;wakaufanya mgongo wako kama ardhi,kama barabara yao ya kupitia.”