1. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Kama nimempa talaka mama yako Yerusalemu,hati ya talaka iko wapi?Au kama niliwauza utumwani,yuko wapi basi, huyo niliyemwuzia?Kumbukeni mliuzwa utumwani kwa maovu yenu,mama yenu alifukuzwa kwa makosa yenu.
2. “Nilipokuja kwa nini sikukuta mtu?Nilipoita mbona hamkuitikia?Je, mkono wangu ni mfupi nisiweze kuwaokoeni?Je, sina nguvu ya kuwakomboa?Tazama! Kwa kuikemea kidogo bahari hukauka,na mito nikaifanya kuwa jangwa,samaki wake wakafa na kunuka kwa kukosa maji.