Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 5:27-30 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Hawachoki wala hawajikwai;hawasinzii wala hawalali;hakuna mshipi wao uliolegeawala kamba ya kiatu iliyokatika.

28. Mishale yao ni mikali sana,pinde zao zimevutwa tayari.Kwato za farasi wao ni ngumu kama mawe;mwendo wa magurudumu ya magari ni kimbunga.

29. Askari wao wananguruma kama simba;wananguruma kama wanasimbaambao wamekamata mawindo yaona kuwapeleka mahali mbaliambapo hakuna awezaye kuwanyanganya.

30. Siku hiyo, watanguruma juu ya Israelikama mvumo wa bahari iliyochafuka.Atakayeiangalia nchi kavuataona giza tupu na dhiki,mwanga utafunikwa na mawingu.

Kusoma sura kamili Isaya 5