Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 5:13-19 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa uhamishonikwa sababu ya utovu wao wa akili.Watu wenu mashuhuri watakufa njaa,watu wengi watakufa kwa kiu.

14. Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa,imepanua kinywa chake mpaka mwisho.Waheshimiwa pamoja na raia wa Yerusalemuwanaingia humo makundi kwa makundi,kadhalika na wote wanaousherehekea.

15. Kila mtu atafedheheshwa,na wenye kiburi wote wataaibishwa.

16. Lakini Mwenyezi-Mungu wa majeshi atatukuzwa.Yeye huonesha ukuu wakekwa matendo yake ya haki,kwa kuwahukumu watu wake.

17. Wanakondoo, wanambuzi na ndama,watapata malisho yao kwenye magofu ya miji yao,kana kwamba hizo ni sehemu za malisho yao.

18. Ole wao wanaoburuta uovu kama kwa kamba;wanaokokota dhambi kama kwa kamba za mkokoteni.

19. Wanasema:“Mwache Mwenyezi-Mungu afanye haraka,tunataka kuyaona aliyosema atayafanya!Mtakatifu wa Israeli na atimize kusudi lake.Hebu na tuone ana mipango gani!”

Kusoma sura kamili Isaya 5