Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 49:23-26 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Wafalme watakushughulikia,na malkia watakutengenezea chakula.Watakusujudia na kukupa heshima,na kuramba vumbi iliyo miguuni pako.Hapo utatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu;wote wanaonitegemea hawataaibika.”

24. Watu wa Yerusalemu walalamika:“Je, shujaa aweza kunyanganywa nyara zake?Au mateka wa mtu katili waweza kuokolewa?”

25. Mwenyezi-Mungu ajibu:“Naam! Hata nyara za shujaa zitachukuliwa,mateka wa mtu katili wataokolewa.Mimi mwenyewe nitawakabili maadui zako,mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.

26. Nitawafanya wanaokukandamiza watafunane;watalewa damu yao wenyewe kama divai.Hapo binadamu wote watatambua kwambamimi ni Mwenyezi-Mungu, Mwokozi wako,mimi ni Mkombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

Kusoma sura kamili Isaya 49