Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 48:7-13 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Mambo hayo yanatukia sasa;hukupata kuyasikia kabla ya leo,hivyo huwezi kusema, ‘Aa! Nilikwisha yajua.’

8. Hujapata kamwe kuyasikia wala kuyajua;tangu zamani masikio yako hayakuyasikia.Nilijua kuwa wewe ni mwenye hila,na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.

9. “Kwa heshima ya jina langu,ninaiahirisha hasira yangu;kwa ajili ya heshima yangu,ninaizuia nisije nikakuangamiza.

10. Mimi nitawajaribu lakini si kama fedha katika tanuri.Nitawajaribu katika tanuri ya taabu.

11. Ninafanya hivyo kwa ajili yangu mwenyewe.Kwa nini jina langu lidharauliwe?Utukufu wangu siwezi kumpa mwingine!

12. “Nisikilize ee taifa la Yakobo,nisikilize ee Israeli niliyekuita.Mimi ndiye Mungu;mimi ni wa kwanza na wa mwisho.

13. Kwa mkono wangu niliuweka msingi wa dunia,mimi mwenyewe nilizitandaza mbingu.Nikiziita mbingu na dunia,zinasimama haraka mbele yangu.

Kusoma sura kamili Isaya 48