4. Kwa ajili ya mtumishi wangu Yakobo,naam, kwa ajili ya mteule wangu Israeli,nimekuita kwa jina lako;nimekupa jina la heshima ingawa wewe hunijui.
5. “Mimi ni Mwenyezi-Mungu, wala hakuna mwingine;hakuna Mungu mwingine ila mimi.Ninakuimarisha ingawa wewe hunijui,
6. ili watu wote, toka mashariki hadi magharibi,wajue kwamba hakuna Mungu mwingine ila mimi;mimi ni Mwenyezi-Mungu na hakuna mwingine.
7. Mimi hufanya mwanga na kuumba giza;huleta fanaka na kusababisha balaa.Mimi Mwenyezi-Mungu hutenda vitu hivi vyote.
8. Enyi mbingu, nyesheni kutoka huko juu,mawingu na yadondoshe uadilifu;dunia na ifunuke, ichipushe wokovu,na kuchanusha uadilifu pia!Mimi, Mwenyezi-Mungu nimefanya hayo.”