Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 45:16-25 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Watengenezaji sanamu wataaibika na kufadhaika,wote kwa pamoja watavurugika.

17. Lakini taifa la Israeli litaokolewa na Mwenyezi-Mungu,litapata wokovu wa milele.Halitaaibishwa wala kufadhaishwa milele.

18. Mwenyezi-Mungu, Mungu pekee,ndiye aliyeiumba dunia,ndiye aliyeiumba na kuitegemeza.Hakuiumba iwe ghasia na tupu,ila aliiumba ikaliwe na viumbe vyake.Yeye asema sasa:“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu,wala hakuna mwingine.

19. Mimi sikunena kwa siri,wala katika nchi yenye giza.Mimi sikuwaambia wazawa wa Yakobowanitafute katika ghasia.Mimi Mwenyezi-Mungu husema ukweli,maneno yangu ni ya kuaminika.”

20. Enyi watu wa mataifa mliosalia,kusanyikeni pamoja mje!Nyinyi mmekosa akili:Nyinyi mwabeba sanamu za mitina kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.

21. Semeni wazi na kutoa hoja zenu;shaurianeni pamoja!Ni nani aliyetangaza zamani matukio ya sasa?Ni nani aliyetamka mambo haya zamani?Je, haikuwa mimi Mwenyezi-Mungu?Hakuna Mungu mwingine ila mimi!Mimi ni Mungu wa haki na mwokozi;hakuna mwingine ila mimi.

22. Nigeukieni mimi mpate kuokolewa,popote mlipo duniani.Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.

23. Mimi nimeapa kwa nafsi yangu,ninachotamka ni ukweli,neno langu halitarudi nyuma:Kila binadamu atanipigia magoti,kila mtu ataapa uaminifu.

24. “Watasema juu yangu,‘Haki na nguvu viko kwa Mwenyezi-Mungu peke yake.’”Wote waliomwakia hasira Mwenyezi-Munguwatamjia yeye na kuaibishwa.

25. Lakini wazawa wa Israeliwatapata ushindi kwake Mwenyezi-Mungu na kufurahi.

Kusoma sura kamili Isaya 45