Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 43:21-28 Biblia Habari Njema (BHN)

21. watu niliowaumba kwa ajili yangu mwenyewe,ili wazitangaze sifa zangu!’

22. “Lakini ewe taifa la Yakobo, hukuniabudu mimi;enyi watu wa Israeli, mlinichoka mimi!

23. Hamjaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa,wala kuniheshimu kwa tambiko zenu.Nami sikuwalemeza kwa kutaka sadaka,wala sikuwachosha kwa kuwadai ubani.

24. Hamkuninunulia manukato kwa faida yenu,wala kuniridhisha kwa nyama nono za tambiko.Badala yake dhambi zenu zimekuwa mzigo kwangu,mmenichosha kabisa kwa makosa yenu.

25. Walakini mimi ndimi niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu,ndimi niyafutaye makosa kwa ajili yangu mwenyewe,na wala sitazikumbuka dhambi zenu.

26. “Niambie kama mna kisa nami,njoo tukahojiane;toeni mashtaka yenu ili tuuone ukweli wenu!

27. Babu yenu wa kwanza alitenda dhambi,wapatanishi wenu waliniasi.

28. Kwa hiyo niliwafanya haramu wakuu wa mahali patakatifunikawaacha watu wa Yakobo waangamizwe,naam, nikawaacha Waisraeli watukanwe.”

Kusoma sura kamili Isaya 43