24. Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota,hata kabla hawajatoa mizizi kama miti udongoni,Mwenyezi-Mungu akiwapulizia hunyauka,kimbunga huwapeperusha kama makapi!
25. Mungu Mtakatifu auliza hivi:“Nani basi, mtakayemlinganisha nami?Je, kuna mtu aliye kama mimi?”
26. Inueni macho yenu juu mbinguni!Je, ni nani aliyeziumba nyota hizo?Ni yule aziongozaye kama jeshi lake,anayeijua idadi yake yote,aziitaye kila moja kwa jina lake.Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi,hakuna hata moja inayokosekana.
27. Enyi watu wa Israeli wazawa wa Yakobo,kwa nini mnalalamika na kusema:“Mwenyezi-Mungu hatujali sisi!Mungu wetu hajali haki yetu!”