Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 40:16-25 Biblia Habari Njema (BHN)

16. Kuni zote za Lebanonina wanyama wake wotehavitoshi kwa sadaka ya kuteketezwa mbele yake.

17. Mataifa yote si kitu mbele yake;kwake ni vitu duni kabisa na batili.

18. Mtamlinganisha Mungu na nini basi,au ni kitu gani cha kumfananisha naye?

19. Je, anafanana na kinyago?Hicho, fundi hukichonga,mfua dhahabu akakipaka dhahabu,na kukitengenezea minyororo ya fedha!

20. Au ni sanamu ya mti mgumu?Hiyo ni ukuni mtu anaochagua,akamtafuta fundi stadi,naye akamchongea sanamu imara!

21. Je, nyinyi bado hamjui?Je, hamjapata kusikia?Je, hamkuambiwa tangu mwanzo?Je, hamjafahamu mwanzo wa dunia?

22. Dunia iliumbwa na huyo aketiye juu ya mbingu;kutoka huko wakazi wa dunia ni kama panzi!Yeye amezitandaza mbingu kama pazia,na kuzikunjua kama hema la kuishi.

23. Yeye huwaporomosha wakuu wenye nguvu,watawala wa dunia huwafanya kuwa si kitu.

24. Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota,hata kabla hawajatoa mizizi kama miti udongoni,Mwenyezi-Mungu akiwapulizia hunyauka,kimbunga huwapeperusha kama makapi!

25. Mungu Mtakatifu auliza hivi:“Nani basi, mtakayemlinganisha nami?Je, kuna mtu aliye kama mimi?”

Kusoma sura kamili Isaya 40