Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 37:20-26 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Sasa ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, utuokoe makuchani mwa Senakeribu, ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe peke yako ndiwe uliye Mwenyezi-Mungu.”

21. Kisha Isaya mwana na Amozi, alituma ujumbe kwa Hezekia akisema, “Hivi ndivyo anavyosema Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli: Kwa kuwa umeniomba kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru,

22. basi huu ndio ujumbe wangu kuhusu huyo mfalme:Mji wa Siyoni, naam, Yerusalemu,unakudharau na kukutukana.Yerusalemu, mji mzuriunakutikisia kichwa kwa dhihaka.

23. Wewe umemtukana nani?Umemkashifu nani?Umethubutu kumbeza nani kwa majivuno?Ni mimi Mungu, Mtakatifu wa Israeli!

24. Umewatumia watumishi wako kunidhihaki mimi Bwana;wewe umesema, ‘Kwa magari yangu mengi ya vita,nimekwea vilele vya milima,mpaka kilele cha Lebanoni.Nimeangusha mierezi yake mirefu,na misonobari mizurimizuri.Nimevifikia vilele vyakena ndani ya misitu yake mikubwa.

25. Nimechimba visima na kunywa maji yake,na nilikausha vijito vya Misrikwa nyayo za miguu yangu.’

26. “Je, hujasikia ewe Senakeribu kwambanilipanga jambo hili tangu zamani?Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.Nilikuweka uifanye miji yenye ngomekuwa rundo la magofu.

Kusoma sura kamili Isaya 37