Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 37:15-30 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Halafu akamwomba Mwenyezi-Mungu akisema;

16. “Ee Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeketi katika kiti cha enzi juu ya viumbe wenye mabawa. Wewe ndiwe uliyeumba mbingu na dunia.

17. Ee, Mwenyezi-Mungu, fumbua macho uone, tega sikio lako, uyasikie matusi yote ambayo Senakeribu amepeleka na kukutukana wewe Mungu uliye hai.

18. Ee Mwenyezi-Mungu, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameangamiza mataifa yote na nchi zao.

19. Waliweza kuitupa miungu yao motoni, kwa sababu haikuwa miungu kweli bali sanamu za miti au mawe zilizochongwa na mikono ya watu.

20. Sasa ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, utuokoe makuchani mwa Senakeribu, ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe peke yako ndiwe uliye Mwenyezi-Mungu.”

21. Kisha Isaya mwana na Amozi, alituma ujumbe kwa Hezekia akisema, “Hivi ndivyo anavyosema Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli: Kwa kuwa umeniomba kuhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru,

22. basi huu ndio ujumbe wangu kuhusu huyo mfalme:Mji wa Siyoni, naam, Yerusalemu,unakudharau na kukutukana.Yerusalemu, mji mzuriunakutikisia kichwa kwa dhihaka.

23. Wewe umemtukana nani?Umemkashifu nani?Umethubutu kumbeza nani kwa majivuno?Ni mimi Mungu, Mtakatifu wa Israeli!

24. Umewatumia watumishi wako kunidhihaki mimi Bwana;wewe umesema, ‘Kwa magari yangu mengi ya vita,nimekwea vilele vya milima,mpaka kilele cha Lebanoni.Nimeangusha mierezi yake mirefu,na misonobari mizurimizuri.Nimevifikia vilele vyakena ndani ya misitu yake mikubwa.

25. Nimechimba visima na kunywa maji yake,na nilikausha vijito vya Misrikwa nyayo za miguu yangu.’

26. “Je, hujasikia ewe Senakeribu kwambanilipanga jambo hili tangu zamani?Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.Nilikuweka uifanye miji yenye ngomekuwa rundo la magofu.

27. Wakazi wake wakiwa wameishiwa nguvu,wametishika na kufadhaika.Wamekuwa kama mimea shambani,kama nyasi changa shambani,kama majani yaotayo juu ya paaau kama ngano kabla hazijakomaaambazo hunyauka upepo mkavu uvumapo.

28. Lakini, nakujua wewe Senakeribu;najua kila unachofanya na kuacha kufanya;najua mipango yako dhidi yangu.

29. Kwa vile umefanya mipango dhidi yanguna nimeusikia ufidhuli wako,nitatia ndoana yangu puani mwako,na lijamu yangu kinywani mwako.Nitakurudisha njia ileile uliyojia.”

30. “Na hii ndiyo itakuwa ishara kwako Hezekia: Mwaka huu na mwaka ujao mtakula kinachomea chenyewe bila kupandwa. Lakini katika mwaka wa tatu mtapanda na kuvuna mavuno; mtapanda mizabibu na kula matunda yake.

Kusoma sura kamili Isaya 37