8. Lakini waungwana hutenda kiungwana,nao hutetea mambo ya kiungwana.
9. Inukeni, enyi wanawake mnaostarehe, mnisikilize;sikilizeni ninayosema enyi mabinti mlioridhika.
10. Katika mwaka mmoja hivi mtatetemeka nyinyi mliotosheka;maana hamtapata mavuno yoyote,na mavuno ya zabibu yatatoweka.
11. Tetemekeni kwa woga, enyi mnaojikalia tu;tetemekeni kwa hofu, enyi mnaostarehe!Vueni nguo zenu, mbaki uchi,mjifunge vazi la gunia viunoni mwenu.
12. Jipigeni vifua kwa huzuni,ombolezeni, kwa sababu ya bustani zilizokuwa nzuri,kwa mizabibu iliyokuwa ikizaa sana,