Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 32:12-20 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Jipigeni vifua kwa huzuni,ombolezeni, kwa sababu ya bustani zilizokuwa nzuri,kwa mizabibu iliyokuwa ikizaa sana,

13. kwa ardhi ya watu wangu inayoota miiba na mbigili,kwa nyumba zote zilizojaa watu wenye furaha,kwa mji uliokuwa na shangwe.

14. Maana ikulu ya mfalme itaachwa mahame,mji huo wa watu wengi utahamwa.Mlima na mnara wa ulinzi utakuwa mapango milele,pundamwitu watapitapita huko kwa furaha,kondoo watapata malisho yao humo.

15. Hali itaendelea kuwa hivyompaka tumiminiwe roho ya Mungu kutoka juu.Hapo jangwa litakuwa shamba la rutuba tena,na mashamba ya rutuba yatakuwa msitu.

16. Haki itadumu katika nchi iliyokuwa nyika,uadilifu utatawala katika mashamba yenye rutuba.

17. Kutokana na uadilifu watu watapata amani,utulivu na usalama utadumu milele.

18. Watu wangu watakaa katika makao ya amani,katika maskani salama na mazingira matulivu.

19. Msitu wa adui utatoweka kabisa,na mji wake utaangamizwa.

20. Lakini heri yenu nyinyi:Mtapanda mbegu zenu popote penye maji,ng'ombe na punda wenu watatembeatembea watakavyo.

Kusoma sura kamili Isaya 32