Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 32:11-16 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Tetemekeni kwa woga, enyi mnaojikalia tu;tetemekeni kwa hofu, enyi mnaostarehe!Vueni nguo zenu, mbaki uchi,mjifunge vazi la gunia viunoni mwenu.

12. Jipigeni vifua kwa huzuni,ombolezeni, kwa sababu ya bustani zilizokuwa nzuri,kwa mizabibu iliyokuwa ikizaa sana,

13. kwa ardhi ya watu wangu inayoota miiba na mbigili,kwa nyumba zote zilizojaa watu wenye furaha,kwa mji uliokuwa na shangwe.

14. Maana ikulu ya mfalme itaachwa mahame,mji huo wa watu wengi utahamwa.Mlima na mnara wa ulinzi utakuwa mapango milele,pundamwitu watapitapita huko kwa furaha,kondoo watapata malisho yao humo.

15. Hali itaendelea kuwa hivyompaka tumiminiwe roho ya Mungu kutoka juu.Hapo jangwa litakuwa shamba la rutuba tena,na mashamba ya rutuba yatakuwa msitu.

16. Haki itadumu katika nchi iliyokuwa nyika,uadilifu utatawala katika mashamba yenye rutuba.

Kusoma sura kamili Isaya 32