Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 32:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kutatokea mfalme atakayetawala kwa uadilifu,nao viongozi wataongoza kwa kufuata haki.

2. Kila mmoja atakuwa kama mahali pa kujikinga na upepo,kama mahali pa kujificha wakati wa tufani.Watakuwa kama vijito vya maji katika nchi kame,kama kivuli cha mwamba mkubwa jangwani.

3. Macho hayatafumbwa tena,masikio yatabaki wazi.

4. Wafanyao mambo kwa hamaki wataamua kwa busara,wenye kigugumizi wataongea sawasawa.

5. Wapumbavu hawataitwa tena waungwana,wala walaghai hawataitwa tena waheshimiwa.

Kusoma sura kamili Isaya 32