Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 3:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Sasa, Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshiataondoa kutoka Yerusalemu na Yuda kila tegemeo:Tegemeo lote la chakula,na tegemeo lote la kinywaji.

2. Ataondoa mashujaa na askari,waamuzi na manabii,waaguzi na wazee,

3. majemadari wa vikosi vya watu hamsini,na watu wenye vyeo,washauri, wachawi stadi na walozi hodari.

4. Mungu ataweka watoto wawatawale;naam, watoto wachanga watawatawala.

5. Watu watadhulumiana,kila mtu na jirani yake;vijana watawadharau wazee wao,na watu duni watapuuza wakuu wao.

6. Wakati huo ndugu atamwambia ndugu yakewakiwa bado nyumbani kwa baba yao:“Wewe unalo koti;utakuwa kiongozi wetu.Chukua hatamu juu ya uharibifu huu!”

7. Lakini siku hiyo atasema,“Mimi siwezi kuwa mwuguzi,nyumbani mwangu hamna chakula wala mavazi.Msinifanye mimi kuwa kiongozi wenu.”

8. Watu wa Yerusalemu wamejikwaa,watu wa Yuda wameanguka,kwa kuwa wanampinga Mwenyezi-Mungukwa maneno na matendo,wakipuuza utukufu wake miongoni mwao.

Kusoma sura kamili Isaya 3