Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 29:15-18 Biblia Habari Njema (BHN)

15. “Ole mnaomficha Mwenyezi-Mungu mipango yenu,mnaotenda matendo yenu gizanina kusema: ‘Hamna atakayetuona;nani awezaye kujua tunachofanya?’

16. Nyinyi mnafanya mambo kinyume kabisa!Je, mfinyanzi na udongo ni hali moja?Chombo hakiwezi kumwambia aliyekitengeneza:‘Wewe hukunitengeneza.’Kilichofinyangwa hakiwezi kumwambia aliyekiumba,‘Wewe hujui chochote.’”

17. Bado kidogo tu,msitu wa Lebanoni utageuzwa kuwa shamba lenye rutuba,na shamba lenye rutuba kuwa msitu.

18. Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa kitabunina kutoka gizani vipofu wataanza kuona.

Kusoma sura kamili Isaya 29