Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 29:12-22 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Na ukimpa mtu yeyote asiyejua kusoma, ukamwambia, “Hebu nisomee kitabu hiki,” atakuambia, “Sijui kusoma.”

13. Bwana asema,“Watu hawa huja kuniabudu kwa maneno matupu,hali mioyo yao iko mbali nami.Wananiheshimu kulingana na mapokeo ya watu tu,jambo walilojifunza wao wenyewe.

14. Hivyo, nitawatenda tena watu hawa maajabu,mambo ya ajabu na ya kushangaza.Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima,na busara ya wenye busara wao itatoweka.

15. “Ole mnaomficha Mwenyezi-Mungu mipango yenu,mnaotenda matendo yenu gizanina kusema: ‘Hamna atakayetuona;nani awezaye kujua tunachofanya?’

16. Nyinyi mnafanya mambo kinyume kabisa!Je, mfinyanzi na udongo ni hali moja?Chombo hakiwezi kumwambia aliyekitengeneza:‘Wewe hukunitengeneza.’Kilichofinyangwa hakiwezi kumwambia aliyekiumba,‘Wewe hujui chochote.’”

17. Bado kidogo tu,msitu wa Lebanoni utageuzwa kuwa shamba lenye rutuba,na shamba lenye rutuba kuwa msitu.

18. Siku hiyo viziwi watasikia ujumbe ukisomwa kitabunina kutoka gizani vipofu wataanza kuona.

19. Wanyofu watapata furaha mpya kwa Mwenyezi-Mungu,na maskini wa watu watashangilia kwa furahakwa sababu ya Mungu, Mtakatifu wa Israeli.

20. Majitu makatili yataangamizwa,wenye kumdhihaki Mungu watakwisha,wote wanaootea kutenda maovu watatokomezwa.

21. Watatoweka wale wanaopotosha kesi ya mtu mahakamani,watu wanaowafanyia hila mahakimuna wasemao uongo kuwanyima haki yao wasio na hatia.

22. Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu aliyemkomboa Abrahamu,asema hivi kuhusu wazawa wa Yakobo:“Wazawa wa Yakobo hawataaibishwa tena,hawatainamisha vichwa vyao tena kwa aibu.

Kusoma sura kamili Isaya 29