1. Ole wako Yerusalemu, madhabahu ya Mungu;mji ambamo Daudi alipiga kambi yake!Miaka yaja na kupita,na sikukuu zako zaendelea kufanyika;
2. lakini mimi Mungu nitauhuzunisha Yerusalemu,nako kutakuwa na vilio na maombolezo,mji wenyewe utakuwa kama madhabahuiliyolowa damu ya watu waliouawa.
3. Mimi nitapanga jeshi dhidi ya Yerusalemu,nami nitauzingira na kuushambulia.
4. Utaangushwa mbali sana ndani ya ardhi;kutoka huko mbali utatoa sauti;maneno yako yatatoka huko chini mavumbini;sauti yako itatoka ardhini kama ya mzimu.