Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 28:3-16 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Majivuno na fahari ya walevi wa Efraimuyatakanyagwakanyagwa ardhini,

4. fahari yake inatoweka kama ua linalonyauka;fahari iliyotawala bondeni kwenye rutubaitakuwa kama tini za mwanzo kabla ya kiangazi;mtu akiziona huzichuma na kuzila mara moja.

5. Siku ile Mwenyezi-Mungu wa majeshi atakuwa taji tukufu,kama kilemba kizuri kwa watu wake watakaobaki hai.

6. Waamuzi mahakamani atawaongoza kutenda haki,nao walinzi wa mji atawapa nguvu.

7. Lakini wako wengine waliolewa divaina kuyumbayumba kwa sababu ya pombe;naam, makuhani na manabii wamelewa mvinyo,wamevurugika kwa divai.Wanayumbayumba kwa pombe kali;maono yao yamepotoka,wanapepesuka katika kutoa hukumu.

8. Meza zote zimetapakaa matapishi,hakuna mahali popote palipo safi.

9. Wao wananidhihaki na kuuliza:“Huyu nabii ataka kumfundisha nani?Je, anadhani atatueleza sisi ujumbe wake?Je, sisi ni watoto wachangawalioachishwa kunyonya juzijuzi?

10. Anatufundisha kama watoto wadogo:Sheria baada ya sheria,mstari baada ya mstari;mara hiki, mara kile!”

11. Haya basi!Mwenyezi-Mungu ataongea na watu hawakwa njia ya watu wa lugha tofautiwanaoongea lugha ngeni.

12. Hata hivyo yeye alikuwa amewaahidi:“Nitawaonesheni pumziko,nitawapeni pumziko enyi mliochoka.Hapa ni mahali pa pumziko.”Lakini wao hawakutaka kunisikiliza.

13. Kwa hiyo kwao neno la Mwenyezi-Mungu litakuwa tu:Sheria sheria, mstari mstari;mara hiki, mara kile!Nao watalazimika kukimbialakini wataanguka nyuma;watavunjika, watanaswa na kutekwa.

14. Basi, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu,enyi wenye madharau mnaotawala watu wa Yerusalemu,

15. “Nyinyi mnajidai mmefanya mkataba na kifo,mmefanya mapatano na Kuzimu!Nyinyi mwasema eti balaa lijapo halitawapata,kwa sababu mmefanya uongo kuwa tegemeo lenu,na udanganyifu kuwa kinga yenu!”

16. Basi, hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi-Mungu:“Tazama! Naweka mjini Siyoni jiwe la msingi,jiwe ambalo limethibitika.Jiwe la pembeni, la thamani,jiwe ambalo ni la msingi thabiti;jiwe lililo na maandishi haya:‘Anayeamini hatatishika.’

Kusoma sura kamili Isaya 28