Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 28:3-10 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Majivuno na fahari ya walevi wa Efraimuyatakanyagwakanyagwa ardhini,

4. fahari yake inatoweka kama ua linalonyauka;fahari iliyotawala bondeni kwenye rutubaitakuwa kama tini za mwanzo kabla ya kiangazi;mtu akiziona huzichuma na kuzila mara moja.

5. Siku ile Mwenyezi-Mungu wa majeshi atakuwa taji tukufu,kama kilemba kizuri kwa watu wake watakaobaki hai.

6. Waamuzi mahakamani atawaongoza kutenda haki,nao walinzi wa mji atawapa nguvu.

7. Lakini wako wengine waliolewa divaina kuyumbayumba kwa sababu ya pombe;naam, makuhani na manabii wamelewa mvinyo,wamevurugika kwa divai.Wanayumbayumba kwa pombe kali;maono yao yamepotoka,wanapepesuka katika kutoa hukumu.

8. Meza zote zimetapakaa matapishi,hakuna mahali popote palipo safi.

9. Wao wananidhihaki na kuuliza:“Huyu nabii ataka kumfundisha nani?Je, anadhani atatueleza sisi ujumbe wake?Je, sisi ni watoto wachangawalioachishwa kunyonya juzijuzi?

10. Anatufundisha kama watoto wadogo:Sheria baada ya sheria,mstari baada ya mstari;mara hiki, mara kile!”

Kusoma sura kamili Isaya 28