Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 26:7-12 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Njia ya watu wanyofu ni rahisi;ewe Mungu mwadilifu, wasawazisha njia yao.

8. Katika njia ya maamuzi yakotunakungojea ee Mwenyezi-Mungu;kulikumbuka jina lako ndiyo tamaa yetu.

9. Moyo wangu wakutamani usiku kucha,nafsi yangu yakutafuta kwa moyo.Utakapoihukumu dunia,watu wote ulimwenguni watajifunza haki.

10. Lakini waovu hata wakipewa fadhili,hawawezi kujifunza kutenda haki.Hata katika nchi ya wanyofu,wao bado wanatenda maovu,wala hawajali ukuu wako wewe Mwenyezi-Mungu.

11. Ee Mwenyezi-Mungu umeinua mkono kuwaadhibu,lakini maadui zako hawauoni.Waoneshe uwapendavyo watu wako nao wataaibika.Moto wa hasira yako uwateketeze maadui zako!

12. Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, umetupatia amani;umefanikisha shughuli zetu zote.

Kusoma sura kamili Isaya 26