3. Maofisa wenu wote walikimbia,wakakamatwa hata kabla ya kufyatua mshale mmoja.Watu wako wote waliopatikana walitekwa,ingawa walikuwa wamekimbilia mbali.
4. Ndiyo maana nawaambieni:Msijali chochote juu yanguniacheni nilie machozi ya uchungu.Msijisumbue kunifarijikwa ajili ya balaa walilopata watu wangu.
5. Maana leo Mwenyezi-Mungu wa majeshiametuletea mchafuko:Kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono.Kuta za mji zimebomolewa,mayowe ya wakazi wake yasikika mpaka milimani.
6. Majeshi ya Elamu, pinde na mishale mikononi,walikuja wamepanda farasi na magari ya vita;nalo jeshi la Kiri lilitayarisha ngao zake.