Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 22:3-6 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Maofisa wenu wote walikimbia,wakakamatwa hata kabla ya kufyatua mshale mmoja.Watu wako wote waliopatikana walitekwa,ingawa walikuwa wamekimbilia mbali.

4. Ndiyo maana nawaambieni:Msijali chochote juu yanguniacheni nilie machozi ya uchungu.Msijisumbue kunifarijikwa ajili ya balaa walilopata watu wangu.

5. Maana leo Mwenyezi-Mungu wa majeshiametuletea mchafuko:Kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono.Kuta za mji zimebomolewa,mayowe ya wakazi wake yasikika mpaka milimani.

6. Majeshi ya Elamu, pinde na mishale mikononi,walikuja wamepanda farasi na magari ya vita;nalo jeshi la Kiri lilitayarisha ngao zake.

Kusoma sura kamili Isaya 22