Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 22:13-19 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Lakini nyinyi mkafurahi na kusherehekea.Mlichinja ng'ombe na kondoo,mkala nyama na kunywa divai.Nyinyi mlisema:“Acha tule na kunywamaana kesho tutakufa.”

14. Mwenyezi-Mungu wa majeshi alinifunulia haya akisema:“Hakika hawatasamehewa uovu huu,watakufa bila kusamehewa.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.”

15. Mwenyezi-Mungu wa majeshi aliniambia niende kwa Shebna, msimamizi wa jamaa ya kifalme, nikamwambie hivi:

16. “Una haki gani kuwa huku? Je, una ndugu yeyote hapa, hata ukajichongea kaburi mwambani juu ya mlima?

17. Wewe ni mwenye nguvu, lakini Mwenyezi-Mungu atakutupilia mbali kwa nguvu.

18. Atakubana kabisa na kukuzungushazungusha, kisha atakutupa kama mpira mpaka katika nchi pana. Huko utafia karibu na magari yako ya vita unayojivunia. Wewe ni aibu kwa nyumba ya bwana wako.

19. Mwenyezi-Mungu atakungoa madarakani mwako na kukuporomosha kutoka mahali ulipo.

Kusoma sura kamili Isaya 22