Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 21:9-17 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Tazama, kikosi kinakuja,wapandafarasi wawiliwawili.Wanasema: “Babuloni umeanguka! Umeanguka!Sanamu zote za miungu yakezimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!”

10. Ewe Israeli, watu wangu,enyi mliotwangwa na kupurwa kama nafaka.Sasa nimewaambieni mambo niliyoyasikiakwa Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli.

11. Kauli ya Mungu dhidi ya Duma.Ninasikia mtu ananiita kutoka Seiri:“Mlinzi, nini kipya leo usiku?Kuna kipya chochote leo usiku?”

12. Nami mlinzi nikajibu:“Asubuhi inakuja, kadhalika na usiku;ukitaka kuuliza, uliza tu;nenda urudi tena.”

13. Kauli ya Mungu dhidi ya Arabia.Enyi misafara ya Dedani,pigeni kambi leo usiku kwenye nyika za Arabia.

14. Enyi wakazi wa nchi ya Tema,wapeni maji hao wenye kiu;wapelekeeni chakula hao wakimbizi.

15. Maana wamekimbia mapanga,mapanga yaliyochomolewa,pinde zilizovutwa na ukali wa mapigano.

16. Maana Bwana aliniambia hivi: “Katika muda wa mwaka mmoja, bila kuzidi wala kupungua, fahari yote ya Kedari itakwisha.

17. Wapiga upinde wachache kati ya mashujaa wa watu wa Kedari ndio watakaosalia. Mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, nimenena.”

Kusoma sura kamili Isaya 21