Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 21:7-11 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Akiona kikosi, wapandafarasi wawiliwawili,wapandangamia na wapandapunda,na awe macho;naam, akae macho!”

8. Kisha huyo mlinzi akapaza sauti:“Bwana, nimesimama juu ya mnara wa ulinzi mchana kutwa,nimeshika zamu usiku kucha!”

9. Tazama, kikosi kinakuja,wapandafarasi wawiliwawili.Wanasema: “Babuloni umeanguka! Umeanguka!Sanamu zote za miungu yakezimetupwa chini na kuvunjwavunjwa!”

10. Ewe Israeli, watu wangu,enyi mliotwangwa na kupurwa kama nafaka.Sasa nimewaambieni mambo niliyoyasikiakwa Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli.

11. Kauli ya Mungu dhidi ya Duma.Ninasikia mtu ananiita kutoka Seiri:“Mlinzi, nini kipya leo usiku?Kuna kipya chochote leo usiku?”

Kusoma sura kamili Isaya 21