Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 18:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ole, wake nchi iliyojaa mvumo wa mabawa,nchi iliyoko ngambo ya mito ya Kushi!

2. Inatuma wajumbe ambao wanasafiri mtoni Nili,wamepanda mashua za mafunjo.Nendeni, enyi wajumbe wepesi,kwa taifa kubwa na hodari,la watu warefu na wa ngozi laini.Watu hao wanaoogopwa kila mahalina nchi yao imegawanywa na mito.

3. Enyi wakazi wote ulimwenguni,nanyi mkaao duniani!Ishara itakapotolewa mlimani, tazameni!Tarumbeta itakapopigwa, sikilizeni.

4. Maana, Mwenyezi-Mungu ameniambia hivi:“Toka makao yangu juu nitatazama yanayotukia,nimetulia kama joto katika mwanga wa jua,kama wingu la umande wakati wa mavuno.

Kusoma sura kamili Isaya 18