Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 17:2-7 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Mitaa yake imeachwa mahame milele.Itakuwa makao ya makundi ya wanyama,wala hakuna mtu atakayewatisha.

3. Ngome za kujihami za Efraimu zitatoweka,na utawala wa Damasko utakwisha.Waashuru ambao watabaki hai,watakuwa na fedheha kama wazawa wa Israeli.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimenena.

4. “Siku hiyo, fahari ya Yakobo itaporomoshwa,na unono wake ataupoteza.

5. Atakwisha kama shamba lililovunwa,atafanyiwa kama mvunaji avunavyo nafaka,atakuwa kama shamba lililovunwa bondeni Refaimu.

6. Atabakiziwa wachache kama vile baada ya zeituni:Zeituni mbili, tatu katika tawi la juu;nne, tano katika matawi ya mti uzaao sana.Mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, nimenena.”

7. Siku hiyo, watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa huyo Mtakatifu wa Israeli.

Kusoma sura kamili Isaya 17