Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 17:11-14 Biblia Habari Njema (BHN)

11. hata mkiifanya ikue siku hiyohiyo mliyoipandana kuifanya ichanue asubuhi hiyohiyo,mavuno yenu yatatowekasiku hiyo ya balaa na maumivu yasiyoponyeka.

12. Lo! Ngurumo ya watu wengi!Wananguruma kama bahari.Lo! Mlio wa watu wa mataifa!Yanatoa mlio kama wa maji mengi.

13. Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi,lakini Mungu atayakemea, nayo yatakimbilia mbali.Yatafukuzwa kama makapi mlimani mbele ya upepo;kama vumbi litimuliwalo na kimbunga.

14. Wakati wa jioni yanaleta hofu kuu,lakini kabla ya asubuhi yametoweka!Hilo ndilo litakalowapata wanaonyakua mali yetu,ndilo litakalowapata wanaotupora.

Kusoma sura kamili Isaya 17