Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 17:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kauli ya Mungu dhidi ya Damasko.“Damasko utakoma kuwa mji;utakuwa rundo la magofu.

2. Mitaa yake imeachwa mahame milele.Itakuwa makao ya makundi ya wanyama,wala hakuna mtu atakayewatisha.

3. Ngome za kujihami za Efraimu zitatoweka,na utawala wa Damasko utakwisha.Waashuru ambao watabaki hai,watakuwa na fedheha kama wazawa wa Israeli.Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimenena.

4. “Siku hiyo, fahari ya Yakobo itaporomoshwa,na unono wake ataupoteza.

5. Atakwisha kama shamba lililovunwa,atafanyiwa kama mvunaji avunavyo nafaka,atakuwa kama shamba lililovunwa bondeni Refaimu.

6. Atabakiziwa wachache kama vile baada ya zeituni:Zeituni mbili, tatu katika tawi la juu;nne, tano katika matawi ya mti uzaao sana.Mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, nimenena.”

7. Siku hiyo, watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa huyo Mtakatifu wa Israeli.

8. Hawatazielekea tena madhabahu ambazo ni kazi za mikono yao wenyewe, wala kuzitazamia tena kazi za mikono yao wenyewe, yaani sanamu za mungu Ashera na madhabahu za kufukizia ubani.

9. Siku hiyo miji yao imara itaachwa mahame, kama miji ambayo Wahivi na Waamori waliihama walipokuwa wakiwakimbia wazawa wa Israeli. Kila kitu kitakuwa uharibifu.

Kusoma sura kamili Isaya 17