Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 13:14-19 Biblia Habari Njema (BHN)

14. “Kama swala anayewindwa,kama kondoo wasio na mchungaji,kila mmoja atajiunga na watu wakekila mtu atakimbilia nchini mwake.

15. Yeyote atakayeonekana atatumbuliwa,atakayekamatwa atauawa kwa upanga.

16. Watoto wao wachanga watapondwapondwa mbele yao,watanyanganywa nyumba zao,na wake zao watanajisiwa.

17. “Ninawachochea Wamedi dhidi yao;watu ambao hawajali fedhawala hawavutiwi na dhahabu.

18. Mishale yao itawaua vijana,hawatakuwa na huruma kwa watoto,wala kuwahurumia watoto wachanga.

19. Babuloni johari ya falme zotena umaarufu wa kiburi cha Wakaldayoutakuwa kama Sodoma na Gomora,wakati Mungu alipoiangamiza.

Kusoma sura kamili Isaya 13