Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 13:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kauli ya Mungu dhidi ya Babuloni ambayo Isaya, mwana wa Amozi, alipewa katika maono:

2. Mungu asema:“Twekeni bendera juu ya mlima usio na miti.Wapaazieni sauti askariwapungieni watu mkonowaingie malango ya mji wa wakuu.

3. Mimi nimewaamuru wateule wangu,nimewaita mashujaa wangu,hao wenye kunitukuza wakishangilia,waje kutekeleza lengo la hasira yangu.”

4. Sikilizeni kelele milimanikama za kundi kubwa la watu!Sikilizeni kelele za falme,na mataifa yanayokusanyika!Mwenyezi-Mungu wa majeshianalikagua jeshi linalokwenda vitani.

5. Wanakuja kutoka nchi za mbali,wanatoka hata miisho ya dunia:Mwenyezi-Mungu na silaha za hasira yakeanakuja kuiangamiza dunia.

Kusoma sura kamili Isaya 13