Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 13:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kauli ya Mungu dhidi ya Babuloni ambayo Isaya, mwana wa Amozi, alipewa katika maono:

2. Mungu asema:“Twekeni bendera juu ya mlima usio na miti.Wapaazieni sauti askariwapungieni watu mkonowaingie malango ya mji wa wakuu.

3. Mimi nimewaamuru wateule wangu,nimewaita mashujaa wangu,hao wenye kunitukuza wakishangilia,waje kutekeleza lengo la hasira yangu.”

4. Sikilizeni kelele milimanikama za kundi kubwa la watu!Sikilizeni kelele za falme,na mataifa yanayokusanyika!Mwenyezi-Mungu wa majeshianalikagua jeshi linalokwenda vitani.

5. Wanakuja kutoka nchi za mbali,wanatoka hata miisho ya dunia:Mwenyezi-Mungu na silaha za hasira yakeanakuja kuiangamiza dunia.

6. Lieni maana siku ya Mwenyezi-Mungu imekaribia;inakuja kama maafa kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu.

7. Kwa hiyo mikono ya kila mtu italegea,kila mtu atakufa moyo.

8. Watu watafadhaika,watashikwa na hofu na maumivu,watakuwa na uchungu kama mama anayejifungua.Watatazamana kwa mashaka,nyuso zao zitawaiva kwa haya.

9. Siku ya Mwenyezi-Mungu inakuja,siku kali, ya ghadhabu na hasira kali.Itaifanya nchi kuwa uharibifu,itawaangamiza wenye dhambi wake.

10. Nyota na vilimia vyake angani hazitaangaza;jua linapochomoza litakuwa giza,na mwezi hautatoa mwanga wake.

Kusoma sura kamili Isaya 13