Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 10:4-10 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Litakalowabakia ni kujikunyata kati ya wafungwana kuangamia pamoja na wanaouawa vitani.Hata hivyo, hasira ya Mwenyezi-Mungu haijatulia,bado ameunyosha mkono wake.

5. Ole wake Ashuru, fimbo ya hasira yangu,yeye ashikaye kiboko cha hasira yangu!

6. Nilimtuma kuliadhibu taifa ovu,nilimwamuru kuwaadhibu watu niliowakasirikia,kuwapora na kuteka nyara,na kuwakanyaga chini kama tope njiani.

7. Lakini Ashuru hakudhamiria hivyo,yeye alikuwa na nia nyingine;alikusudia kuharibu kabisa,kuangamiza mataifa mengi iwezekanavyo.

8. Maana alisema:“Je, si kweli majemadari wangu ni wafalme?

9. Je, si kweli kwamba Kalno nitautenda kama Karkemishi,mji wa Hamathi kama mji wa Arpadi,Samaria kama Damasko?

10. Kama nimefaulu kuunyosha mkono wangudhidi ya falme zenye sanamu za miungukubwa kuliko sanamu za Yerusalemu na Samaria;

Kusoma sura kamili Isaya 10