Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 10:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Ole wao wanaotunga sheria zisizo za haki,watu wanaopitisha sheria za kukandamiza.

2. Huwanyima maskini haki zao,na kuwaibia maskini wa watu wangu maslahi yao.Wajane wamekuwa nyara kwao;yatima wamekuwa mawindo yao.

3. Je, mtafanya nini siku ya adhabu,siku dhoruba itakapowajieni kutoka mbali?Mtamkimbilia nani kuomba msaada?Mtakwenda wapi kuweka mali yenu?

Kusoma sura kamili Isaya 10